Msanii wa filamu, Gabo Zigamba ametoa ya
moyoni kuhusu mapungufu ambayo yanafanya filamu za Tanzania kutofanya
vizuri katika nchi kubwa hasa zile za kimaitafa.
Akizungumza na Ayo TV alisema….‘Pungufu
la mwanzo kabisa linatokana na bajeti kuwa ndogo kwahiyo tukianza na
bajeti ikiwa ndogo lazima kuna vitu vitatu au vinne vikafanywa na mmoja
kwahiyo tayari itakuwa upungufu mwingine kwa maana ya kwamba director
anaweza akawa yeye ndo producer‘- Gabo
‘kwahiyo
kazi ya watu wawili au kazi ya watu watatu ikafanywa na mtu mmoja
upungufu unakuwa mkubwa sana na cinema inakuwa sio nzuri mwisho wa siku
haifanyi vizuri kimataifa’- Gabo
0 comments:
Post a Comment